google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Aug 21, 2017

Hata Kama Mambo Kwako Ni Magumu…Bado Hujachelewa Kufikia Mafanikio Yako.

No comments :
Kama unafikiri umechelewa kufanya kile unachotakiwa kukifanya elewa hivi…
Mpaka sasa kitabu kizuri bado hakijaandikwa…
Mpaka sasa nyimbo nzuri kuliko zote duniani bado haijaimbwa,..
Mpaka sasa jengo zuri zaidi duniani bado mpaka dakika hii halijajengwa…
Mpaka sasa chakula kizuri kuliko vyote bado hakijapikwa…
Mpaka sasa ugunduzi mkubwa kuliko yote duniani bado haujafanyika unasubiriwa…
Mpaka sasa mashine safi na ya kisasa bado haijagunduliwa…
Mpaka sasa mfanyabiashara mkubwa kuliko wote duniani wa karne bado hajatokea…
Mpaka sasa mwandishi bora wa vitabu kuliko wote na wakati wote bado hajaibuka…
Mpaka sasa mafanikio yote makubwa yapo yanakusubiri wewe…
Narudia mpaka sasa mafanikio hayo makubwa yapo yanakusubiri wewe…
Huhitaji kutilia shaka uwezo wako, tumia maarifa yako kutoa yaliyobora…
Hakuna kinachoshindikana chini ya dunia, ikiwa utaamua…
Ndani mwako una nafasi ya kutoa mafanikio yoyote ukiamua…
Kipi kinachokuzuia, mafanikio makubwa wakati wote bado hayajatokea…
Je, unataka kujiona unakata tamaa na kujiona tena basi…
Usijione uko hivyo, unayo nafasi ya kubadilisha kila kitu kwenye maisha yako…
Unayo mbegu ya mafanikio makubwa ndani mwako, itumie…
Wewe ni bora na unaweza kuibadilisha dunia…
Usikubali kufa kifo cha mende miguu juu kwa kufikiri huwezi…
Unaweza, huo uwezo unao, na inawezekana…
Bado hujachelewa hata kama mambo ni magumu...
Tumia muda wako vizuri...tumia nafasi uliyonayo vizuri...utafanikiwa...
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kujifunza kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
 Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.