google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 7, 2017

Dakika Tano Tu, Zinatosha Kukamilisha Mpango Huu Mkubwa Kwako.

No comments :
Dakika tano ni dakika chache sana ambazo kila mtu anaweza akazipuuzia na kuona hakuna cha maana unachoweza kukifanya kwa dakika hizo.
Watu wengi ikiwamo hata wewe, huona dakika tano ni kidogo na kuamua kuzipotezea hata pale inapotokea wana umiliki wa dakika hizo tano au chini ya hapo.
Ninachotaka kukwambia ipo faida na muujiza mkubwa ambao utaupata kwenye maisha yako ikiwa utakubali kutumia kila dakika tano kubali maisha yako.
Naona unashangaa na kujiuliza hili linawezekana vipi? Ipo namna ambayo unaweza ukafanya na kubadili maisha yako kwa kutumia dakika tano ulizonazo.

Tumia muda wako vizuri ukupe mafanikio.
Kwa mfano, ni dakika tano tu zinatosha kabisa kukutuliza kutoka kwenye hasira na kutulia hadi kushindwa kufanya maamuzi ya hasira.
Ni dakika tano pia ambazo unaweza ukaamua kufanya jambo ulitaka kuriahirisha na kuamua kufanya kwa dakika tano tu basi.
Ni dakika tano tu zinakutosha kuanza kuanza kufanya kazi yoyote ambayo ilikuwa na ugumu na mwisho wa siku ikawa nyepesi.
Hapa unaona kabisa dakika tano zinaweza zikabadilisha hali fulani ambayo ilikuwa mbovu na ikawa nzuri.
Kwa hiyo hapa ninachoka unielewe ni hivi,,kwa chochote kile unachotaka kukifanya lakini unaona kuna ugumu fulani jipe dakaka tano za mwanzo.
Usikubali kuacha jambo hilo likaishia hewani, kubali kweli kuna ugumu na umechoka na huwezi kufanya, lakini jipe dakika tano tu za kufanya kidogo.
Inawezekana kuna kitabu unataka kusoma lakini unaona uvivu, usikubali na wewe ukaacha kabisa, jipe dakika tano tu za kuanza kusoma kwanza.
Kwa kujipa dakika tano hiyo itakusaidia kuweza kupata ‘momentum’ mpya itakayokufanya uweze kusonga mbele kila wakati.
Kwa kutumia dakika tano tu, utagundua kwamba itakusaidia kutoka kwenye tabia za hovyo zinazo kukwamisha hadi kwenda kwenye tabia za mafanikio.
Kikubwa unachotakiwa kuelewa hapa, kujipa dakika tano za kufanya jambo lolote unalolifanya, itakusaidia sana kukufanikishia mipango yako mingi.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.