google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 14, 2017

Zijue Mbinu Za Kuijenga Kesho Yako, Yenye Mafanikio.

No comments :
Hivi ni nani aijuaye kesho yake? Kiimani ukiulizwa swali kama hili huenda ukakosa majibu sahihi, hii ni kwa sababu wengi wetu hakuna ambaye aijuae kesho yake. Lakini katika sayari ya upangaji malengo na kanuni ya mafanikio ni lazima kila mmoja wetu aijue kesho yake.

Hii ni kwa sababu ni lazima kila mmoja wetu  aweze kujua ni wapi ambapo anaelekea katika maisha yake, hii ikiwa na maana ya kwamba kama mtu ataamua kuyapanga malengo yake katika misingi imara ni lazima kila mmoja wetu ataijua kesho yake ipoje.

Wakati mwingine ili uweze kuwa bora katika maisha yako ya kila siku unatakiwa kuweza kujua ni jinsi gani ya kuitengeneza kesho yako. Na mbinu za kuitengeneza kesho yako mara zote huanza na siku leo, swali la msingi la kujiuliza ni kwamba unaitumia vipi leo yako ili kuijenga kesho yako?

Kesho yako ya mafanikio inatengenezwa leo.
Kama utashindwa kuijua leo yako vizuri basi fahamu fika hata hiyo kesho yako huwezi kuijua pia. Hivyo jambo la muhimu ambalo unatakiwa kulifanya ni kuhakikisha unaijenga kesho, ni unaijenga tabia ambayo itakufanya kesho yako iwe ni nzuri.  Miongoni mwa tabia ambazo unatakiwa kuziacha ni pamoja na kuacha kufanya mambo ambayo yatakuwa hayana msaada wowote kwako.

Lakini mara baada ya kuuachana na tabia ambazo zimekuwa hazikusaidia, lakini jambo jingine ni kuhakikisha unafanya mambo ambayo yatakufanya wewe uweze kusonga mbele katika maisha yako yako ya kila siku ili kuijenga kesho yako nzuri.

Hivyo ni  vyema ukatafakari kwa makini ni mambo gani ambayo hayakusaidii, mara baada ya kujua mambo hayo chukua peni na karatasi kisha yaorodheshe kisha anza kufanya kinyume chake cha mambo hayo.

Kama ulikuwa unatumia muda mwingi kwenye kusoma vitu visivyokuwa vya msingi basi kuanzia sasa ni vyema ukatenga muda wako katika kusoma vitu ambavyo vitakusaidia. Kama ulikuwa unachelewa kuamka pasipo na sababu maalum basi anza pia kufanya kinyume chake.

Mara zote ili uweze kuijenga kesho yako unachotakiwa kufanya hakikisha ya kwamba unafanya mambo kwa uhakika na ustadi wa hali juu. Kila unachokifanya ni vyema ukatumia ile kanuni ya kwenda mbele zaidi.

Kama ni biashara ni lazima ujifunze kufanya vitu ambavyo vitakufanya uweze kusonga mbele, achana na tabia ambazo zimekuwa hazileti matokeo chanya.

Mpaka kufikia hapo sina la ziada nikutakie siku njema na mafanikio mema.

Ndimi ; BENSON CHONYA
0757-909942.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.