google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 9, 2017

Umezaliwa Ili Kufanya Mambo Haya Tu…

No comments :
Kila siku iitwapo leo, yapo mambo makubwa yanayokamilishwa  ikiwemo ndoto na mipango na watu wenye sifa kama za kwako.
Tunaona viwanda vikubwa, miradi mikubwa inagunduliwa na watu wenye changamoto na wanaoishi mazingira kama yale yale uliyonao wewe.
Pia hata ukiangalia mabadiliko ya kisayasansi yanayotokea kila siku na kuubadilisha ulimwengu, yanasababishwa pia na watu wale wale wenye sifa kama za kwako.
Mpaka hapo unaona hiyo yote inadhihirisha au inakuhakikishia kwamba, binadamu umezaliwa kwa kusudi moja tu la kufanya mambo makubwa.

Kama ulikuwa umefika mahali unajidharau na kujiona wewe kama ni panzi utakuwa unakosea sana, hujazaliwa uwe hivyo hata kidogo.
Umezaliwa kuweza kufanya mapinduzi makubwa sana kwenye maisha yako na maisha ya wengine pia.
Unatakiwa kuujua uwezo mkubwa uliondani mwako. Kwa kuujua uwezo huo ulio ndan mwako inakusaidia sana kuleta mabadiliko ya kweli na makubwa.
Kwa sasa tunaishi katika dunia ambayo ina uwezo wa kutupa mabadiliko na mafanikio yoyote tunayatakayo.
Usiangalie hali ya kipato chako au maisha yako yalivyo kwa sasa, unachatakiwa kujua kwamba unaweza kufanya mabadikilo makubwa sana na ya kushangaza.
Umezaliwa kufanya makubwa hapa duniani. Kama kila wakati umekuwa ukiwazia kufanya mipango midogo midogo hiyo sio saizi yako.
Unachotakiwa kufanya ni kubadilisha msimamo wako mara moja na kuelekea upande mwingine wa kufanya makubwa.
Kufanya yaliyo makubwa kwenye maisha yako, hakutokani na pesa  ni matokeao ya kuamua kwanza na kujua ni wapi unakotaka kufika.kimaisha.
Unayo nafasi ya kufanya maisha yako ya hapa duniani yakawa bora kama wewe unavyotaka yawe. Hakuna mtu wa kukuzuia katika hilo.
Muda wa kuanza kufanya yale yaliyo makubwa katika maisha yako ni sasa. Hutakiwi kusubiri kesho au lini, huu ndio muda wako.
Ipo miradi mikubwa sana ambayo inakusubiri wewe uikamilishe. Ikiwa utacheza hutaweza kufanikisha kitu chochote.
Msisitizo ninaotaka ujue hapa katika makala haya ni kwamba, wewe umezaliwa kwa kufanya mambo makubwa na sio kinyume chake.
Kwa hiyo asikudanganye mtu eti huwezi au wewe ni mdogo sana, unayo nafasi ya kuweza kufika mbali kimafanikio kwa kufanya yaliyo makubwa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.