google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 16, 2017

Maisha Yako Yanajengwa Sana Na Mambo Haya Matatu.

No comments :
Yapo mambo mengi ambayo yanajenga maisha yako au yanafanya maisha yako yawe kama hivyo yalivyo. Lakini hata hivyo pamoja na mambo hayo mengi, yapo mambo matatu ya msingi ambayo yanajenga maisha yako au ndio msingi wa maisha yako.
Kama utapuuzia ama hautaweza kujali mambo hayo matatu tu, basi kufanikiwa kwako kutakuwa ni kitu ambacho hakiwezekani. Mimi na wewe tunatengeneza mafanikio au kushindwa kwetu kupitia mambo hayo.
Sina shaka, una hamu ya kutaka kujua ni mambo gani ambayo yanapelekea maisha yako kujengwa. Sasa kamata kalamu na karatasi, kisha twende pamoja kwenye darasa kuweza kujifunza somo letu la leo.
Jambo la kwanza, mawazo yako.
Kila kitu unachokitaka kinaanzia kwenye mawazo yako. Hakuna jambo ambalo lipo duniani limeanzia nje ya mawazo. Mawazo yana mchango mkubwa katika kukupa chochote ukitakacho kwenye maisha yako.
Ukishindwa katika mawazo yako, na nje utashindwa pia. Ndio maana ili kufanikiwa unatakiwa kila wakati uwe na mawazo chanya sana, mawazo yakujenga, mawazo ambayo yatakutoa sehemu moja na kukupeleka sehemu nyingine.
Na mawazo haya hayawezi kuja kwa bahati mabya tu, mawazo haya yanakuja kwa wewe kujilisha vitu chanya karibu kila siku. Unatakiwa ujifunze vitu chanya, unatakiwa uwe na marafiki chanya ambao watakusaidia kuwa na mawazo bora.
Kuendelea kuwa na mawazo yale yale ambayo yamekuweka hapo ulipo, ni sawa na kuchagua kupotea kwenye maisha yako. Kila siku hakikisha una mawazo bora yatakayoweza kukusaidia wewe kufanikiwa na si kukuangusha.

Jambo la pili, vitendo vyako.
Mawazo bora peke yake hata yawe mazuri vipi hayawezi kukusaidia kitu au hayawezi kukufikisha mbali. Kitu kingine ambacho kinajenga maisha yako kwa sehemu kubwa ni hatua unazozichukua kila siku.
Inatakiwa ujiulize hatua unazochukua kila siku hata kama ni kidogo sana lakini katika kuelekea ndoto zako ni zipi? Kama hakuna hatua unazochukua basi ujue sio unajenga maisha yako bali ndio unayaharibu kabisa na kuwa maisha ya hovyo.
Hakuna mafanikio ya kukaa tu, hakuna mafanikio ya kuyaongelea mdomoni, mafanikio yanajengwa kwa kuchukua hatua. Ukiona hakuna hatua unazochukua usijidanganye kwamba unatafuta na wewe mafanikio, maana wewe utakwama hata iweje.
Watu wanaochukua hatua karibu kila siku, watu hao ndio wanaofanikiwa na kujenga bahati kubwa katika maisha yao. Kwa hiyo unaona, vitendo ni kitu kimojawapo ambacho kina mchango mkubwa sana pia katika kujenga maisha yako.
Jambo la tatu, maneno yako.
Pamoja na kwamba una mawazo mawazo mazuri na una vitendo vizuri, lakini unatakiwa kukumbuka maneno yako pia yanamchango mkubwa sana katika kujenga maisha yako na yakaonekana kama hivyo yalivyo hapo.
Maisha ya wengi yamejengwa au kuharibiwa kutokana na maneno yao waliojinenea siku za nyuma. Ndio maana kabla hujaongea inabidi ujiulize unaongea kitu gani na je kitu hicho kinamchango upi katika kuelekea ndoto zako.
Unaweza ukawa mtabiri wa maisha yako, eidha kwa kwa kubomoa au kuyaumba. Maneno yako yanaumba sana maisha yako kwa sehemu kubwa. Ukijinenea vibaya, uelewe kabisa ndivyo maisha yako yataharibika kabisa.
Hivyo ni muhimu kuwa na uchaguzi wa maneno bora ili ikusaidie kuweza kufanikia. Usiwe mtabiri wa kuharibu maisha yako kila wakati. Jifunze kuwa mtabiri wa kuweza kukusaidia kujenga maisha yako.
Kwa kifupi, hayo ndiyo mambo makubwa matatu ambayo yanajenga maisha yako sana, ingawa ukienda kinyume na hapo ndivyo unaharibu maisha yako kabisa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.