google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 11, 2017

Jinsi Ya Kuifanya Siku Yako Iwe Ya Mafanikio Na Hamasa Kubwa Sana.

No comments :
Yapo mambo ya wazi ambayo yanaweza yakaifanya siku yako ikapotea na ukaishia kufanya mambo ambayo hayakusaidii kabisa. Inapotokea ukaiendesha siku yako bila faida hiyo ni hasara kubwa sana kwako.
Na mambo kuharibika katika siku yako hadi kupelekea siku yako kuharibika na kuwa ya hovyo huwa haianzi mbali sana. Mambo yote huwa yanaanzia kwenye lile saa la kwanza unapoamka. Saa hili la kwanza ni muhimu sana kwako.
Huo muda au saa hilo ni wakati wa wewe kutulia na kulitumia vizuri hadi kufikia mafanikio. Ikiwa lakini saa hilo moja utalitumia hovyo ujue kabisa utakwama na utaharibu karibu kila kitu katika siku yako ambayo ilitakiwa iwe ya mafanikio kwako.
Kwa kuwa rafiki tupo pamoja na sipendi siku yako ikaishia kuwa ya kushindwa kila siku, ipo namna ambayo unatakiwa ujue unaweza ukaifanya siku yako ikawa ya mafanikio na hamasa kubwa. Kivipi hili linaweza likafanikiwa?
1. Jifunze vitu vipya.
Unaweza ukaaamua katika saa moja lako la kwanza la siku, ikawa ni wakati wako wa kujifunza vitu vipya. Huu ni wakati ambao akili yako inakuwa ina nguvu sana na kufanya kitu chochote na inakuwa rahisi kuweza kuelewa.
Kwa kuanza na kujifunza vitu vipya asubuhi na mapema hiyo itakusaidia sana kukuza au kujenga misuli yako ya kimafanikio. Wengi hawawezi kufanya hili na matokeo yao huanza na kusoma meseji kwenye simu au ‘kuchat’ na kujibu email za watu.
Kuanza siku yako na vitu ambavyo havikusaidii huko ni sawa na kujipoteza. Kama umeamua kusoma asubuhi kwa ajili ya kuongeze maarifa yako, muda huu usiwe nao na machezo hata kidogo, sema kweli kwa faida yako.

2. Fanya mazoezi.
Asubuhi na mapema kabla siku yako haijanza au kabla hujaanza kujihusisha na mambo mengine, pia wakati huu unaweza ukatenga dakika chache za kufanya mazoezi ya mwili. Unatakiwa kuelewa mazoezi ni kitu cha muhimu sana kwako.
Unapofanya mazoezi yanaifanya akili yako iwe na hamasa ya kutenda vitu vingi. Kama una tabia ya kufanya mazoezi, angalia siku ambayo ulifanya mazoezi ulikuwaje na pia angalia ile au zile siku ambazo hukufanya mazoezi ulikuwaje?
Sina shaka utagundua siku ambazo hukufanya mazoezi ulikuwa hovyo sana. Na ile siku ambao ulifanya mazoezi akili yako ilikuwa iko sawa. hivyo unaona mazoezi ni mojawapo ya kitu ambacho kinaweza kikaipa siku yako hamasa kubwa.
3. Andika.
Kama wewe ni mwandishi au hata kama sio mwandishi, ianze siku yako pia kwa kuamua kuandika. Andika yale unayojifunza kupitia vitabu au yale unayojifunza kupitia maisha ya wengine pia.
Kumbukumbu ni kitu cha muhimu sana katika maisha yako leo na hata kesho. Kumbukumbu unazoweka zinakusaidia wewe kwa leo na hata kwa baadae. Lakini si hivyo tu, zinawasaidia na wengine kila wakiona kile unachokiandika.
Na kwa jinsi unavyoandika inakusaidia hata wewe kujifunza na mwisho wa siku utajikuta umeainza siku yako kwa ubora kabisa kwa sababu kutakuwa kuna kitu ambacho umekikamilisha na pia inakusaidia kutoa ‘stress’.
4. Pitia mambo ya msingi.
Asubuhi na mapema ni wakati wa wewe kupitia mambo yako ya msingi. Usianze siku yako kwa kupiga tu simu au kujibu meseji eidha iwe kwa ‘whats app’ au ‘email’, hao utakuwa unaharibu siku yako.
Unashauriwa kitaalamu moja ya jambo unalotakiwa kulifanya asubuhi kabisa ni kwa wewe kupitia yale mambo ya msingi, yaani kupitia vipaumbele vyako ulivyo navyo. Kwa kufanya hivyo kila kitu kitakuwa kinakwenda kwako kwa mpangilio.
Kwa kujifunza mambo hayo, itakusaidia sana wewe kuweza kuifanya siku yako ikaanza kwa hamasa na mafanikio makubwa.
Fanyia kazi hayo na kwa makala nyingine za mafanikio kumbuka kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Blog; dirayamafanikio.blogspot.com
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,
Email; dirayamafanikio@gmail.com
                                                              



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.