google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 17, 2017

Sababu Tano Kwanini Watu Wengi Hawafanyi Kazi Zao Kwa Ufanisi Mkubwa.

No comments :
Si kitu cha ajabu, mara nyingi kumekuwa na malalamiko mengi kwa ‘mabosi,’ kulalamikia watu walio chini yao kwamba wanafanya kazi chini ya viwango, lakini si hivyo tu bali wanafanya pia kwa ufanisi mdogo sana, yaani hakuna ubora.
Ni tatizo ambalo limekuwa likiongelewa sana na kuhusishwa na uvivu, kwamba vijana wa siku hizi ni wavivu na hawataki kufanya kazi sana na tatizo hili limekua likikua siku hadi siku katika maeneo mengi makazini.
Je, kwa wewe binafsi, unafikiri chanzo cha tatizo hili ni nini? Kwa nini watu wanakwenda kazini karibu kila siku, lakini utendaji na ufanisi wao ni kidogo sana na hata hauridhishi kwa kiasi kikubwa kuweza kuleta mabadiliko.
Kiuhalisia zipo sababu kadhaa, ambazo moja kwa moja zinakuwa zinapelekea utendaji wa kazi kuweza kushuka sana kazini. Sitaki kukutajia sababu nyingi sana, katika somo hili nakutajia sababu tatu tu, kwa nini watu wengi hawafanyi kazi zao kwa ufanisi.
1. Mwingiliano wa mambo yasiyo ya msingi.
Ufanisi wa kazi kuna wakati unapungua sana kutokana na kuingiliana kwa mambo yasiyo ya msingi. Kwa mfano, utakuta mtu anafana kazi moja lakini wakati huo huo akili yake ipo kwenye kitu kingine kama simu au Tv au kuongea na watu wakati wa kazi.
Ufanisi katika kazi na kufanya kazi katika ubora hakuwezi kuja kwa namna hii. Ndio maana unatakiwa kila aina ya mwingiliano uweze kuutoa ili ufanisi uweze kuonekana kwa uwazi kabisa kwenye kila unachokifanya.
Sababu hii peke yake, ni chanzo kikubwa sana cha watu wengi kutokufanya kazi kwa ufanisi mkubwa. Matokeo ya hili ni kuendeleza kushindwa kwenye maisha. Kama unataka kufanya kazi kwa ufanisi na kufanikiwa, punguza mwingiliano wa mambo yasiyo ya msingi kwako.

2. Kazi nyingi kwa wakati mmoja.
Pia kuna wakati ufanisi katika kazi unakufa kwa sababu ya kazi nyingi kwa wakati mmoja. Inapofika kipindi wewe ni mtu mmoja halafu ukawa na kazi nyingi kwa wakati mmoja ni ngumu sana kuweza kuleta ufanisi.
Kitu cha muhimu kuzingatia hapa, ni kufanya kazi zako kwa utaratibu. Usijipe kazi nyingi kwa wakati mmoja, huko kutakuwa ni kujichosha na utapoteza ufanisi sana na usishangae hutaweza kupiga hatua kwa jambo hata moja.
Siri kubwa ya kuweza kufanikiwa na kusonga mbele, chagua jambo moja na kisha jambo hiilo lifanye kwa uhakika sana. Nguvu na mawazo yako yote yaweke hapo mpaka jambo lako lilete matokeo na ufanisi mkubwa sana.
3. Kukosa hamasa kutoka kwa wanaowaongoza.
Kuna wakati kama unafanya kazi kwenye kampuni yaani uko chini ya mtu, unaweza ukakosa ufanisi kwa sababu ya kukosa hamasa kutoka kwa wanaokuongoza. Ni muhimu sana kwa watu wanaokuongoza au viongiozi wakatoa hamasa kubwa.
Pengine unajiuliza hamasa hii ni ipi? Ni muhimu na kwa viongozi pia nao kuweza kujitoa kufanya kazi ili kuonyesha mfano. Kinyume cha hapo unaweza ukakatishwa tamaa kwa kujiona kama hiyo kazi unayoifanya ni kazi yako tu peke yako.
Lakini kwa kushirikiana pamoja kuanzia viongozi hadi wafanyakazi wa kawaida ingawa kila mtu anakuwa anafanya kazi kwa sehemu yake hiyo itasaidia kukupa motisha na mwisho wa siku kuleta ufanisi mkubwa katika kazi.
Kimsingi, hayo ndiyo mambo makubwa matatu ambayo yanapelekea moja kwa moja watu kuweza kufanya kazi chini ya ufanisi mkubwa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,







No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.