google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 26, 2017

Hutakiwi Kukwepa Jambo Hili Kama Unataka Kufanikiwa Kwa Kishindo.

No comments :
Vipo vitu vingi katika safari yako ya mafanikio ambavyo hutakiwi kivikwepa hata kidogo kama unataka kufika juu sana kwenye mafanikio. Ila kama unataka kufika kwenye mafanikio ya kawaida tu, unaweza ukavikwepa tu hakuna hata shida.
Leo sitataka kuzungumzia sana vitu vingi, naomba nikudokezee jambo moja tu ambalo  unatakiwa kutolikwepa ila unatakiwa ujue namna ya kukabiliana nalo ili uweze kufanikiwa kwa kishindo kikubwa.
Jambo hili si lingine bali ni kubeba hali hatarishi au kukabiliana na hali yoyote hatarishi ili kuweza kufanikiwa. Unaweza ukawa hujanielewa vizuri lakini ninachomaanisha hapa ni kuchukua ‘risk’ ili uweze kufanikiwa. Mpaka hapo sina shaka tupo pamoja.

Ukumbuke maisha yamejaa kila aina ya hali hatarishi. Huwezi kukwepa kukutana na hali yoyote hatarishi katika maisha yako. Ukikwepa hali hii ni lazima utakutana na hali nyingine hatarishi ambayo unatakiwa kupambana nayo mpaka kuweza kuishinda.
Kama kila wakati unaogopa kujitoa mhanga kwa sababu ya kuogopa kujihatarisha, basi tambua hapo ni sawa na kuchagua umeshindwa. Hutaweza kufika popote kama hauko tayari kuchukua ‘risk’ yoyote inayokupeleka kwenye ndoto yako.
Inatakiwa ujitoe mhanga kweli, haijalishi unajitoa mhanga kwenye kitu gani, kwenye malengo yako uliyojiwekea au kwenye kitu kingine chochote. Swala la kujitoa mhanga nakukubali kupoteza baadhi ya vitu ili ufanikiwe unatakiwa kulijua kwa ufasaha sana.
Maarifa uliyonayo unayatakiwa kuyatumia ili kukabiliana na kila aina ya changamoto na si kukimbia changamoto yoyote ile. Kukimbia changamoto na kuogopa kujihatarisha hiyo inaweza ikawa ni sawa na ujinga kwako ambao utakunyima mafanikio.
Unaweza ukajiuliza ni kitu gani ambacho utakipata hapa dunia pasipo wewe kuweza kujihatarisha. Ukisema biashara ni lazima uweke muda na pesa zako ili upate kile unachokitaka. Ukiangalia karibu kila kitu kwanza lazima uhatarishe ndio upate.
Kwa mfano hata wewe, umezaliwa kwa kujihatarisha pia. Uhai ulionao vilevile wewe kama wewe hauna uhakika nao, hiyo yote bado unaishi katika hali hatarishi. Hiyo kama iko hivyo kwa nini usiamue ukubali kujihatarisha kwa chochote ili ufanikiwe.?
Mara nyingi kuchukua ‘risk’ kwa kile unachotaka kukifanya, mwisho wa siku huweza kukupa wewe unayechukua ‘risk’ hiyo zawadi kubwa ya mafanikio. Ukumbuke tu mafanikio yote yanaanza kupatikana kwa wewe kuchukua ‘risk’ na sio kinyume chake.
Kwa hiyo badala ya kukimbia hali hatarishi yoyote kwako, unatakiwa kujua namna ya kuweza kukabilina nayo ili uweze kufanikiwa. Kama hautafanya hivyo utashindwa tu hata ufanyaje, hutaweza kukwepa kushindwa.
Ukumbuke kama nilivyokwambia mafanikio yanapatikana kwa wale watu ambao wanajitoa mhanga sana yaani kwa watu wanaochukua ‘risk’ kama wewe si miongoni mwao sahau kidogo kuhusu kufanikiwa, waache wachukua ‘risk’ wafanikiwe.
Kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji kuuziwa vifaranga bora na kwa bei nafuu, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.