google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 4, 2017

Jifunze Mfumo Huu Wa S2C Ili Kuikuza Biashara Yako.

No comments :
Ukitaka kufanikiwa kibiashara ni lazima uweze kubuni njia mbalimbali ambazo zitakusaidia wewe uweze kuwa mfanyabiashara bora, huwezi kusema unataka kufanikiwa katika biashara halafu njia ambazo unataka kuzitumia ni njia za kihenga.
Ninaposema njia za kihenga sijui unanielewa kweli? Maana yangu ni kwamba njia za kihenga ni zile mbinu za ufanyaji wa biashara ambazo zimekwisha pitwa na wakati na zimekuwa hazileti matokeo ya haraka.
Njia hizo ni pamoja na kususubiria mteja akafuate sehemu ambayo unafanyia biashara. Njia hii ni njia ya kihenga sana na kama bado unaitumia njia hii basi fahamu fika unajichelewesha wewe mwenyewe.

Wafuate wateja wako kule waliko.
Hivyo kila wakati ni vyema ukatumia mfumo unaitwa S2C, seller to costomer. Mbinu hii ni mfumo mpya wa kuuza bidhaa ambao unamuwezesha muuzaji kumfuta mteja mahali alipo. Nasisitiza juu ya kuitumia mbinu hii kwa kuwa matokeo yake ni ya haraka zaidi katika kuleta mageuzi ya kibiashara.
Nasema hivi nikiwa na maana binadamu ameumbwa na hulka ya matumizi ya ghafla pindi aonapo kitu kizuri machoni pake, hivyo kama utatumia njia hii ya kumfuta mteja mahali alipo kuna uhakika kwa asilimia zote za binadamu huyo kununua kitu ambacho hakupanga kukinunua ili mradi tu uweze kuwa na uwezo mkubwa wa kumshawishi mteja huyo.
Hebu jaribu kutafakari wale ambao hufanya kazi ya kunadi biashara zao katika mabasi ya abiria, hivi wale wateja ambao huwa wananua zile bidhaa ni kwamba walipanga kununua bidhaa hizo? Majibu ya maswali hayo utagundua ya kwamba hapana hawakupanga kununua bidhaa hizo bali wamejikuta wakivutiwa na bidhaa au huduma fulani ya ghafla.
Achilia mbali wafanyabiashara wa kwenye magari hepu tuwaangalie wale vijana ambao huzunguka mitaani kwa ajili ya kusajili la laini za simu, swali la kujiliza je, wanachokipata ni sawa na kama wangekaa sehemu zao za kazi? usinipe jibu.
Niache bla bla nisije poteza maana yangu ya leo, ila nilichotaka kukwambia ni kwamba jenga utaratibu wa kumfuata mteja mahali alipo kwani kufanya hivyo ni njia bora ya kuongeza mauzo katika biashara yako.
Faida nyingine ambayo utaipata kwa kutumia njia hii ya kumfuta mteja  ni kwamba utakuwa na mahusiano mazuri na wateja wako, kwani wateja wako watakuwa wanakufahamu zaidi. Hata pale ambao watahitaji huduma yako itakuwa ni rahisi kukupata kwa sababu umekuwa na hulka ya kiwatembelea wateja hao mara kwa mara.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ndimi afisa mipango wa mafanikio yako.
Benson Chonya,
Mawasiliano; +255 909 942,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.