google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 10, 2017

Jinsi unavyoweza Kujua Vipaumbele Vyako Vya Kweli.

No comments :
Ipo namna rahisi ambayo inaweza kukusaidia kujua vipaumbele vyako vya kweli na hata vipaumbele vya mtu mwingine bila hata kuambiwa. Nasema vipaumbele vya kweli kwa sababu, unaweza ukawa na vipaumbele, lakini usipochukua hatua, hivyo sio vipaumbele vya kweli.
Najua unaelewa kila mtu anasema  ana vipaumbele vya aina fulani na wengine vipaumbele hivyo huwa wana vitaja kwa kuvipamba sana. Kitu cha kujiuliza je, hivyo vipaumbele vyao wanavifatilia na kuchukua hatua?
Kama nilivyosema ni rahisi kusema tu, ‘ooh mimi nitafanya, hiki au kile kwa sababu ndio kipaumbele changu’.  Sawa hatukatai, lakini hata useme vipi, unaweza ukasema sana lakini mwisho wa siku vipaumbele vyako visiwe hivyo ambavyo unaviongelea.

Ndiyo, unashangaa, ni kweli kabisa, unaweza ukaongea sana vipaumbele vyako ni hivi, lakini visiwe hivyo tena, kivipi hili?tutajua kutokana na utekelezaji wako, unatekeleza kitu gani, nini ambacho unakifanya? Hapo  ndipo kipaumbele chako kilipo.
Inabidi ufike mahali uelewe, vipaumbele vyako vinaonekana si kwa kile unachokisema tu, bali vipaumbele vinaonekana kwa jinsi namna unavyochukua hatua zako. Yale mambo unayoyachukulia hatua na kuyafanikisha ndiyo yanaonyesha vipaumbele vyako halisi.
Ukitaka kujua vizuri vipaumbele vyako ni vipi, angalia vitu vinavyokuzunguka,  ni kitu gani ambacho umekamilisha na kitu gani ambacho hujakamilisha. Vile vyote ulivyovikamilisha iwe kwa mwaka huu au miaka ya nyuma, ndivyo vipaumbele vyako ulikuwa navyo.
Kwa hiyo ili kujua vipaumbele vya mtu huhitaji sana kusikia kile anachokisema kwa mdomo wake, angalia vile alivyovikamilisha au subiri ni kitu gani ataanza kukikamilisha hicho ndicho kilikuwa kipaumbele chake cha muhimu.
Unaweza ukawa una vipaumbele vizuri sana kwa kuviongea, lakini katika utekelezaji hivyo basi visiwe vipaumbe vyako. Vipaumbele vizuri sana kwa upande wako ni vile ambavyo vimeshaingia kwenye mchakato au vile unavyovifanyia kazi.
Vipaumbele unavyojiwekea au ulivyo navyo ni zaidi ya ile orodha ambayo unaiandika. Unatakiwa ujifunze vipaumbele halisi vinapatokana kwa wewe kuweza kuchukua hatua kamili kwenye maisha yako na sio kusema peke yake.
Kama kuna mahali unaona huridhiki na maisha  yako na unapata matokeo ambayo sivyo, inatakiwa ubadili vipaumbele vyako kwa kuweza kuchukua  hatua zinazositahili na si kuishia kusema tu peke yake.
Inatakiwa ukumbuke, vipaumbele vya kweli kwenye maisha yako ambavyo vitakuletea matokeo chanya uyatakayo vinakuja kwa wewe kuweka juhudi ,vinakuja kwa wewe kukabiliana na kila aina ya changamoto na kujitoa hadi kuweza kufanikiwa.
Vipaumbele hivi kwa wenzetu wazungu  wanaviita ‘unspoken priorites’, yaani vipaumbele vinavyojieleza vyenyewe, vipaumbele ambavyo huhitaji kuviongelea sana ila matokeo yanaonekana moja kwa moja kwa nje na kwa uwazi mkubwa.
Ukweli ni kwamba, umewahi na unaweza kuwa na viapumbele vya kweli ambavyo itakusaidia kubadili maisha yako. Siri ya kweli ya kubadili maisha yako ni kuwa na vipaumbele vya kweli va kubadili mfumo wa maisha yako.
Umeona kama tulivyonaza kusema kwenye makala hii, vipaumbele vya kweli vinakuja kwa wewe kuchukua hatua, kujitoa na hadi kuona unafanikisha ndoto zako na lakini sio kuishia kusema sema tu kwamba hivi ni vipaumbele vyangu.
Hivyo, unachotakiwa kufanya wewe ni kupiga kazi na kuacha vipaumbele vya kweli viseme vyevyewe. Huhitaji kuwaambia watu sana vipaumbele vyako vya kweli ni vipi au pia huhitaji kuuliza vipaumbele vyako vya kweli ni vipi, utajua tu kwa yale wanayoyafanya.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.