google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 5, 2017

Jenga Mtazamo Huu, Ukusaidie Kufanikiwa Kwa Asilimia Mia Moja.

No comments :
Watu wenye mafanikio wanaishi katika dunia moja na watu ambao hawana mafanikio. Maisha na mazingira wanayoishi watu wenye mafanikio na watu ambao hawana mafanikio, yanafanana kwa sehemu kubwa sana.
Kwa mfano, utakuta watu wasio na mafanikio wanaishi kwenye mazingira na changamoto nyingi kama kukatishwa tamaa, kukataliwa sana, lakini cha ajabu hata watu wenye mafanikio pia, wanaishi kwenye mazingira kama hayo hayo.
Unaweza ukafikiri kiraisi sana eti tu kwa sababu wewe huna pesa au kwa sababu wewe una changamoto nyingi, basi unajiona wewe una dunia yako na wale watu wenye mafanikio wana kama dunia yao. Hakuna kitu kama hicho.

Tengeneza mtazamo chanya ukusaidie kufanikiwa.
Wote tunaishi katika dunia ile ile yenye jua  lile lile na changamoto zile zile. Pengine mpaka hapo unajiuliza sasa kama iko hivyo ni kitu gani ambacho kinatofautisha watu wenye mafanikio na watu ambao hawana mafanikio?
Kiuhalisia, yapo mambo mengi yanayofanya wewe ushindwe na wengine wafanikiwe ingawa mazingira wote mnaishi ya kufanana. Kitu kimojawapo kinachokufanya ushindwe ni namna wewe unavyochukulia mambo.
Haijalishi ni hali gani uliyonayo au ni kitu gani ambacho kinachokukumba, ila jinsi unachokulia mambo nako ni muhimu sana kwa mafanikio yako. Kila jambo unatakiwa kulichukulia kwa uchanya zaidi hata kama limekujia vibaya.
Ni kweli sikatai changamoto katika maisha zipo na nyingi tu, lakini unapokutana na changamoto hizo unakuwa unazichukuliaje? Je, unajiona changamoto hizo zinakuzamisha au unaona nini?
Kama nilivyosema ni muhimu sana kuwa na mtazamo mzuri kwa kila kitu kinachokutokea yaani unatakiwa kuwa na ‘positive success response’ nzuri ambayo itakusaidia kufanikiwa. Ikiwa unachukulia mambo hovyo na wewe utakuwa hovyo tu.
Watu wote wanaochukulia mambo kwa mtazamo chanya, watu hawa ni watu wa mafanikio kila wakati. Uwe na uhakika utafanikiwa kwa asilimia zote kama kila kitu unakichukulia kwa mtazamo chanya.
Hata mambo yako yanapokwama unakuwa unaelewa, ipo siku mambo yangu yatakaa sawa, hiyo ndiyo imani kubwa unakuwa nayo na unashangaa kweli unafanikiwa kuweza kufikia mafanikio yako.
Kila wakati zingatia kuwa na mtazamo chanya katika maisha yako na utafanikiwa karibu kwa kila jambo, ikiwa mtazamo huo utauendeleza karibu  siku zote kwenye maisha yako. Mtazamo chanya ni njia sahihi ya mafanikio yako.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,






No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.