google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Nov 1, 2017

Matunzo Ya Kuku Wanaotaga.

No comments :
Hapa tunaangalia majogoo na mitetea yenye umri wa kuanzia miezi minne na kuendelea.

Matunzo mengi wanayopewa ni sawa na ya kuku wanaokua (tafadhali rejea kwenye somo la matunzo ya kuku wanaokua).

Matunzo mengine ya ziada:-

1. Watenge majogoo na matetea kwa idadi inayofaa. 

Kama unafuga huria, jogoo mmoja kwa mitetea 6.

Kama unafuga kwenye vyumba, jogoo mmoja kwa mitetea 4-5.

2. Wape chakula cha ‘layers’ chenye virutubisho vya kutosha. 

3. Endelea kuchanja Newcastle kila baada ya wiki 10.


 4. Endelea kuwapa dawa ya minyoo kila baada ya wiki 10.

5. Walishe majani na mboga mboga kwa wingi, ili mayai watakayotaga yawe na kiini cha njano. 

6. Kuwa makini sana na sehemu ya kifua na eneo la chini la mitetea, ambapo ndipo mayai yanapohifadhiwa kwa ndani. Kuku akigongwa au akijigonga eneo hilo,  yai linaweza kupasuka kwa ndani, na tetea huyo atanyong'onyea, na baada ya siku kadhaa atakufa. 

7. Okota mayai mara nyingi iwezekanavyo, ili kuzuia kuku kula mayai au wasiyavunje au kuyawekea ufa. 

8. Kuku wanapoanza kutaga nunua daftari ya kutunza kumbukumbu za mayai yanayotagwa kila siku. Hii itakusaidia kujua siku wanapopunguza kutaga, ili kutafuta chanzo, na kama ni ugonjwa, watibiwe haraka.

Kila la kheri katika ufugaji wako, na endelea kuwa pamoja nasi katika masomo mengine ya ufugaji wa kuku.

Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji kuuziwa vifaranga bora na kwa bei nafuu, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO na PURE KIENYEJI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,



No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.