google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 31, 2017

Kama Unafikiri Mafanikio Utayapata Kwa Njia Hii, Sahau.

No comments :
Kujenga nidhamu binafsi na kuishi maisha unayoyataka wewe sio kitu rahisi kinachotokea tu mara moja.
Kujitoa na kufanya yale yanayotakiwa kufanyika ili kuweza kutimiza ndoto zako, halikadhalika hicho nacho si kitu rahisi.
Kuweza kutimiza ahadi zako na kuwa na mawazo zingativu juu ya ndoto zako pia nacho hicho si kitu rahisi kuweza kukufanikisha kama unavyofikiri.
Kupanga mipango yako na kufanyia kazi ili iweze kutoa mafanikio pia hicho sio kitu rahisi, kuna ugumu fulani unaojitokeza.

Ukiangalia katika maisha karibu kila kitu ambacho unataka kukifanya na kweli kikatoa mafanikio, kina ugumu wa aina fulani hivi.
Ukiona kuna jambo ukilifanya ni mteremko sana kwako na halihitaji wewe  kujibidiisha sana, ujue hapo kufanikiwa si rahisi sana pia.
Utaona mpaka hapo mafanikio yanahitaji nguvu na kujitoa sana kila wakati  na kila siku ili uweze kuyafikia.
Lakini ikiwa utaamua kuyaendea mafanikio kwa mkono wako mlegevu au kwa jinsi unavyotaka wewe kufanikiwa kwako itakuwa ni shida.
Hapa sina shaka unapata picha kamili kwamba hakuna kitu rahisi katika hii dunia. Kila kitu kina ugumu wake katika kukipata.
Ukiona mtu anakwambia mafanikio ni rahisi au wewe mwenyewe unaona mafanikio ya mwingine yamepatikana kama kwa urahisi vile, sio kweli.
Ipo namna yule mtu ambaye labda unamuona kafanikiwa kiurahisi kapigana na kuweza kufanikiwa kwa mafanikio yale.
Lakini ukiwa na ndoto za kufanikiwa huku umelala, na bila kijibiidisha vya kutosha andika utaumia hutaweza kufanikiwa popote.
Amua kwenye maisha yako kutenga muda wa kutafuta mafanikio yako, kubali kupigika kiakili, kimwili lakini usikubali ukashindwa kufanikiwa.
Unajua dunia tunayoishi ina kila kitu cha kukupa mafanikio. Kinachosababisha ukose mafanikio ni juhudi na nguvu zako tu na sio kitu kingine.
Kama unataka mali na pesa hizo zipo, lakini sio rahisi kuzipata, unatakiwa uweke juhudi na kufanya kazi kwa nguvu zote na kuachana na mchezo mchezo.
Kama utacheza na huku unasema unatafuta mafanikio makubwa, nikwambie tu ukweli huo ni uongo, ambao tena labda unajidanganya wewe na kuwadanganya na wengine pia.
Elewa hauna kitu ambacho cha kimafanikio ni rajisi katika maisha yako, ipo nguvu ambayo unatakiwa kuitumia ili kupata kitu chochote kile.
Chochote kile ambacho kinakupa mafanikio au chochote kile ambacho kinabadili tabia au hali yako na kuwa bora si rahisi sana kukipata.
Kama unafikiri mafanikio utayapata kwa njia ya urahisi, sahau. Unatakiwa kuweka juhudi kwa nguvu zako zote.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.