google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 29, 2017

Acha Kuendelea Kufanya Kosa Hili Tena Na Tena Unapotafuta Mafanikio Yako.

No comments :
Kati ya kosa ambalo hutakiwi kuendelea kulifanya kwenye maisha ni kufanya vitu au mambo yako kwa kuingia na mawazo ya kujaribu.
Hili ni kosa kubwa ambalo linawangusha wengi wanaposema wanataka kufanya kitu fulani halafu wanasema hebu ngoja ni jaribu.
Unajua unaposema najaribu maanake nini?  hiyo ina maana hicho kitu ambacho unakifanya kwanza huna uhakika nacho kama utakiweza.
Kwa hiyo unapojaribu, usitegemee kama kuna ushindi wowote unaweza ukatokea, maana wewe si unajaribu.

Wale wote wanaojaribu sio rahisi kuweza kufanikiwa kupata ushindi, kwa sababu akili na kila kitu kinakuwa kimekaa kwa kujaribu jaribu.
Unapotaka kufanya jambo halafu ukaingia na mawazo ya kujaribu, kwanza hata ukishindwa unakuwa hauna uchungu sana, kwa sababu utasema ulikuwa unajaribu.
Pia hata hivyo, utakuwa ni mtu ambaye una sababu hata  kama ukishindwa, lazima utasema tu si nilikuwa najribu tu sio nilikuwa nafanya kabisa.
Kwenye maisha hakuna uwanja wa majaribio hata siku moja. Kama unafanya kitu au vitu vyako kwa kujaribu unajipotezea muda wako bure na unajidanganya.
Ikiwa kama kuna vitu umeamua kuvifanya, jitoe kufanya vitu hivyo kwa ukamilifu wako wote lakini sio kufanya majaribio.
Wakati wewe utaendeleakuendeleza wimbo wa kujaribu, wapo watu ambao wamejitoa kufanya kweli kwenye maisha yao na hawajaribu.
Najua hili ni kosa ambao umekuwa ukilifanya sana na limekuwa likagharimu maisha yako lakini si wakati wa kuweza kurudia tena.
Kimefika kipindi cha kusimamia ndoto zako, kimefika kipindi cha kuhakikisha ndoto zako zinaweza kutimia na kuwa kweli.
Jaribu kujiuliza utaendelea kujaribu mpaka lini? Jipe muda wa kufanya mambo yako, achana na habari ya kujaribu maisha hayakusubiri hata kidogo.
Washindi katika maisha ni watu wa kufanya na si watu wa majaribio. Chagua kufanya kitu hata kama ni kidogo sana lakini kifanye na usijaribu hata kidogo.
Kujaribu mara nyingi kunakuandalia mazingira ya wewe kuweza kushindwa moja kwa moja. Hakuna mafanikio utakayoweza kuyapata kwa kuishi maisha ya kujaribu.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.