google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 27, 2017

Kipe Kipaumbele Kitu Hichi Kikupe Mafanikio.

No comments :
Hivi umeshawahi kujiuliza au unajua ni kitu gani ambacho ni cha muhimu sana kwenye maisha yako? je, ni afya, familia, imani yako au ni kitu gani?
Iwe kwa kujua au kutokujua kwa kawaida kipo kitu cha muhimu sana karibu kwa kila mtu kwenye maisha yake. Kitu hicho ndicho kinacho ongoza maisha ya mtu huyo.
Hata hivyo pia, kila siku maisha yanatuuliza kitu cha muhimu kwetu, na kwa bahati nzuri tunajibu kupitia vitendo vyetu na si midomo.
Kwa mantiki hiyo, hata nikikuuliza kitu kipi cha muhimu kwako hata usiponijibu najua vitendo vyako vitanijibu vizuri sana kuliko maneno yako.

Zipo namna nyingi amabazo zinaweza kukusaidia kujua kipi ni cha muhimu kwako au kwenye maisha yako na kipi si cha muhimu.
Unaweza kujua kitu cha muhimu kwako kwa kuangalia jinsi unavyotumia muda wako kufanya jambo fulani hivi.
Ikiwa muda wako umeutenga kufanya jambo fulani na kila siku na  jambo hilo unalifanya na huachi basi hicho ni kitu cha muhimu sana kwako na kina matokeo.
Chochote kile unachokipa muda wako mwingi hicho ndicho kitu cha muhimu bila kujali kitu hicho kina faida au hakina.
Inawezekana kabisa kitu cha muhimu kwako ikawa ni maongezi au kufatilia habari na inawezekana pia kitu cha muhimu kwako ikawa ni kufatilia ndoto zako.
Kitu kipi kitakachotufanya tujue kitu kipi cha muhimu kwako ni kwa jinsi wewe unavyotenga muda wako kwenye kitu hicho kila wakati.
Ukumbuke kitu cha muhimu kwako inaweza ikawa hata kuimba, kuangalia mpira ila kama kina kula muda wako basi hicho ndicho kitu cha muhimu kwako.
Maisha yako yako hivyo kutokana na kuna vitu ambavyo ulivipa umuhimu hivyo vitu ndivyo vimefanya uwe na maisha hayo.
Sasa ikiwa ulikuwa unatumia muda wako mwingi kwa vitu vya hovyo hovyo itakugharimu na kwa sababu havijakusaidia kitu.
Kuanzia leo, anza kufanya vitu vya muhimu kwako ili vikusaidie kukupa mafanikio bora leo na kesho kwenye maisha yako yote.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,




No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.