google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 6, 2017

Tafuta Majibu Ya Kitu Hiki Utafanikiwa.

No comments :
Wakati mwingine inawezekana ukawa ni kinara mzuri wa kulalama juu ya maisha yako, huku ukisahau ya kwamba unachokizungumza mara kwa mara ndicho ambacho kinasabaisha maisha hayo kuwa magumu zaidi.
Mara nyingine mdomo huumba hicho unachokizungumza, mara kadhaa nimekuwa nikiwasikia vijana kwa wazee wakisema vyuma vimekaza, hii ikiwa ina maana ya kwamba mambo ni magumu sana, wapo wengine ambao wanasema ya kwamba  jamaa anabana, sijui ni jamaa gani?
Swali linakuja ni kwanini umeyaruhusu maisha yako yaongozwe na fikra za aina hii?
Nasema hivi nikiwa kifua mbele pasina kuona aibu, nikiwa  na maana ya kwamba, watu wengi tupo vizuri sana katika kuzungumza matatizo yaliyopo kuliko kuzungumza suluhisho la matatizo hayo.
Yupo mwanafalsafa mmoja aliwahi kusema katika maandiko yake ya kwamba, acha kuzungumza kuhusu matatizo bali zungumza kuhusu suluhisho la matatizo hayo, kwani kutumia muda mwingi kuzungumzia kuhusu matatizo ni kuongeza matatizo na si kupata majawabu.

Tafuta majibu ya changamoto zako.
Hebu tujiulize wale wote wanaozungumzia matatizo ya ajira pasina kutafuta majibu ya suluhisho la suala hilo wapo wapi? Je tatizo limeisha au ndo kwamba limezidi? Majibu unayo wewe mpenzi msomaji wa makala haya. Maana yangu ni kwamba laiti tungekuwa tunazungumza majibu ya tatizo la ajira, huenda tungekuwa tulishapata majibu ya tatizo hili. Najaribu kuwaza kwa sauti.
Suala la vyuma kukaza pamoja na jamaa kubana ni kubaki kuzungumzia matatatizo, japo hata kama ukweli unaona upo hivyo, unachotakiwa kufanya ni kutafuta majibu ya vyuma hivyo kukaza na si kubaki kuendelea kulizungumzia masuala hayo pasina kutafuta suluhisho.
Mara nyingi katika maisha yako ya kila siku huna budi kujifunza kuwa chanya, haijalishi maisha ni magumu kiasi gani ambayo unayapitia. Na sifa kuu ya mtu kuwa chanya si kuungana na watu wengine kushabikia vitu ambavyo havina msaada wowote katika maisha yako, bali ni kusimama kidete wewe kama wewe kwani maisha yako uyajue ni wewe.
Pamoja na hali ya kiuchumi kubadilika kama wengi wasemavyo, kwa kuwa  wewe ni mtu chanya na kama nilivyosema hapo awali uache mara moja  tabia ya kuzungumzia masuala ya matatizo bali jifunze kutafuta majibu ya matatizo hayo.
Hivyo kila wakati, kila saa na kila muda jijengee utaratibu na mfumo thabiti wa kutafuta majibu ya changamoto zinazokubali, kwani kufanya hivi ni kujenga utaratibu mpya na mwanzo wa wewe kuweza kufanikiwa zaidi.
Mwisho ni nimalizie kwa kusema “usizungumzie hapo ulipo bali zungumza kitu ambacho unataka kukifanya hapo baadae, kisha uweke mipango thabiti ya kulitenda jambo hilo kwa wakati huu.
Imeandikwa na Afisa Mipango Benson Chonya,
0757909942.

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.