google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 24, 2017

Kitu Hiki Ndicho Kitakachokufanya Ukue Sana Kimafanikio.

No comments :
Kitu chochote kinachokupa changamoto wewe, ni kitu hicho hicho ndicho kinachokufanya ukue na ujenge ukomavu kutokana na changamto unazopitia.
Unapokuwa unakutana na changamoto hizo, uwezo wako wa kutenda unaongezeka na unakuwa ni mtu mwingine hata mara baada ya kuvuka changamoto hizo.
Mara nyingi changamoto zinapoanza na kutokea kwenye maisha ya mtu ni mbaya sana, lakini kwa kiasi kikubwa zinasaidia kumpa mtu ukomavu.
Kwa mfano, kama unatembea kawaida huwezi kuwa sawa na yule anayepanda milima. Kwa vyovyote mpanda mlima ni rahisi kujenga misuli mikubwa ya mwili kuliko asiyepanda.

Changamoto ipi inayokukabili wewe? Changamoto hiyo kumbuka ndiyo inayokupa uzoefu na ukomavu mkubwa utakao kupa mafanikio yakutosha.
Watu wote wenye mafanikio makubwa, watu ambao ukiwaangalia wamefika mbali sana kimafanikio ni watu ambao wanapambana sana na changamoto kwenye maisha yao.
Huwezi kufanikiwa na kufika juu sana kwenye mafanikio yako kama wewe ni mtu wa kutoroka au kukimbia changamoto kila wakati.
Unatakiwa ufike wakati ujue ni kwa jinsi gani utakavyoweza kukabiliana na changamoto ili ziweze kukupa ushindi wa kimafanikio.
Changamoto kwenye mafanikio ni silaha au njia nzuri sana ya kuweza kukusaidia wewe kuweza kufanikiwa au kufika mbali kimafanikio.
Ulimwengu una changamoto sana, ni changamoto hizo ndizo ambazo ukijua namna ya kukabiliana nazo zitakupa mafanikio makubwa sana.
Hakuna namna au hakuna mtu ambaye ana uwezo wa kuzikimbia changamoto. Uwe una pesa au huna, changamoto katika maisha zipo palepale.
Acha kuwaona watu wengine ni kama watu ambao maisha yao mazuri sana hayapitii kwenye changamoto zozote, changamoto kila mtu anazipitia na ndizo ziletazo mafanikio.
Kuwa miongoni miongoni mwa watu ambao wataamua kukua kutokana na changamoto wanazo kabiliana nazo kila siku.
Lakini ikiwa kila unapokutana na changamoto unalalamika sana au unaamua kukimbia kufanikiwa kwako itakuwa ni vigumu.
Washindi katika maisha wanakumbana na changamoto nyingi sana ambazo mwisho wa siku huwaacha wakiwa washindi kutokana na kuzishinda changamoto hizo.
Kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.

Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji kuuziwa vifaranga bora na kwa bei nafuu, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na bei kwa kila kifaranga ni tsh. 1800/=. Wote manakaribishwa.

Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.