google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Oct 21, 2017

Siri Ya Kupata Zaidi Kile Ukitakacho.

No comments :
Ni tabia au asili ya binadamu kila anachokipata kutaka kukipata zaidi na zaidi. Hapa yaani binadamu anakuwa ana shauku ya kupata kwa wingi zaidi.
Tabia au asili hii wewe unayo na mimi ninayo na kila aliye binadamu ili mradi anahema tu tabia hiyo anayo na anaitumia pia.
Kinachokuja kutofautisha ni matakwa ya utakaji wa vitu hivyo. Utakuta kila mtu anapenda kitu ambacho ni tofauti au hakifanani sana na mwingine ili kiwe kingi.
Kwa mfano, wapo wanaopenda wawe na mali au pesa kwa wingi, wapo pia wanaopenda wawe waimbaji wazuri na bora kabisa.
Pia wapo wale wanaopenda kupata idadi kubwa ya watu wanaowafatilia/ ‘followers’ hasa wasanii na wale watu ambao ni watumiaji wazuri wa mitandao ya kijamii.

Kila mtu kama nilivyosema kipo kitu ambacho anataka kiongezeke na kuwa kingi kabisa na kutokana na hilo, hufanya kila linawezekana kukiongeza kitu hicho.
Kutaka kile ulichonacho kiendelee kuongezeka sio jambo baya ni jambo zuri, lakini badala ya kuwa na shauku hiyo tu peke yake, unachotakiwa kufanya, ongeza juhudi.
Unajiuliza uongeze juhudi wapi? Ongeza juhudi ya kufanya zaidi kwa kile kitu ulichonacho au unachokifaya ili kikusaidie kupata mambo mengine zaidi.
Najua vizuri sana kuna kitu fulani unakifanya, kitu hicho kinaweza kikawa kidogo na kisikupe hamasa sana, lakini unatakiwa kuongeza juhudi ili kujenga mafanikio zaidi.
Hakuna kitachoweza kukusaidia kupata kitu unachokitaka kwa wingi zaidi kama hutaweka juhudi kwa unachokifanya. Juhudi yako itakupa matunda.
Ila kama unafikiri kila wakati unataka zaidi, kiuhalisia utaanza kujiona huna kitu kabisa, utaanza kuona maisha yako yapo tupu na huna kitu kabisa.
Ndio maana nasema unataka kupata kitu zaidi weka juhudi kwa unachokifanya ili kikusaidie kupata zaidi na zaidi.
Kuendelea kufikiri makubwa unayotaka bila kuweka juhudi utakuwa unatengeneza nguvu za kukufanya wewe mwenyewe ukashindwa kufikia malengo yako.
Acha kuendelea kuweka nguvu za mawazo yako kwa yale mambo ambayo hauna, weka juhudi kwa kile ukifanyacho, nguvu hizo zitakupa mambo makubwa.
Kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji kuuziwa vifaranga bora na kwa bei nafuu, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO na PURE KIENYEJI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na bei kwa kila kifaranga ni tsh. 1800/=. Wote mnakaribishwa.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.