google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 26, 2018

Hata Kama Unaona Unashindwa Sana, Ipo Sehemu Hii Yenye Ushindi Wako.

No comments :
Pamoja na kwamba maisha yana changamoto nyingi sana, lakini kipo kitu cha kijifunza kupitia changamoto hizo hata kama zinakukatisha tamaa sana.
Pamoja na kwamba unaweza kudondoka au ukashindwa kwa namna fulani kwenye maisha yako, lakini upo uwezekano wa kuamka na ukawa mshindi tena.
Pamoja na kwamba unaweza ukapata hasara sana kwenye biashara au chochote kile ukifanyacho, lakini upo uwezekano wa kupata faida iliyo kubwa tena.
Pamoja na kwamba kuna kukakatishwa sana tamaa kwenye maisha yako, lakini tambua tumaini la kukuwezesha kusonga mbele kwenye mafanikio uyatakayo lipo.

Ushindi wa mafanikio yako upo, ukiamua.
Pamoja na kwamba umekuwa ukikosea na kufanya mambo mengi kwa njia ambayo si sahihi, lakini upo wakati ambao utaweza kufanya mambo yako kwa usahihi pia.
Unachopaswa kuelewa hapa ni kwamba, kwa sura yoyote ile ambayo maisha yanakujia, hata kama ni kwa sura mbaya, tambua ushindi upo.
Huhitaji kulia, huhitaji kulalamika sana kwamba maisha yako ni hovyo sana, upo upande wa pili ambako kuna ushindi wako pia.
Hata inapotokea hali unaona kama umekandamizwa na maisha, huwezi kunyanyuka, nikwambie tu uwezekano wa kunyanyuka tena upo, unatakiwa kulijua hilo akilini mwako.
Kitu kikubwa unachotakiwa kuelewa, kama upo kwenye upande wa kushindwa, unatakiwa kufanya jitihada za kuwa kwenye upande wa ushindi kimafanikio.
Maisha hayapo kwenye upande wa ubaya tu, maisha yana pande mbili, upande wa hasi na upande wa chanya ambao ni ushindi.
Kwa hiyo kila unapoona kama dunia inakuonea au unajiona kuna vitu umekosa kabisa, unatakiwa kukumbuka upo wakati utakuwa huru na hautaweza kuonewa.
Unatakiwa uondokane na fikra za kufikiri sana ubaya katika maisha yako, mambo yakija kinyume na ulivyotarajia, ujue ushindi pia upo.
Upo upande wa ushindi, upo upande ambao unatakiwa uufanyie kazi na uweze kushinda kwenye safari ya mafanikio.
Upande wa mafanikio upo, hilo unatakiwa kulijua kila wakati, nakukumbusha tena hutakiwi kukata tamaa au kujiona huwezi tena, mafanikio yako yapo.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.