google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 31, 2018

Mawazo Yanayofanya Maisha Yako Yabadilike Ni Haya Hapa.

No comments :
Maisha uliyonayo mara nyingi sana ni matokeo ya yale mawazo ambayo unayo wewe. Uumbaji wa maisha yako yawe ya mafanikio au kushindwa, unaanza na mawazo.
Mawazo ndiyo chanzo cha uhalisia ambao unaona kwa nje. Kitu chochote unachokiona, kabla hakijawa hivyo, kilianza kama mawazo.
Mawazo yako yanapoanzia, hayaanzii sehemu nyingine zaidi kwenye akili. Hapa nikiwa na maana akili yako ndiyo inayotengenezea uhalisia wa matokeo ya nje.
Hiyo ikiwa na maana, chochote kile unachokiweka kwenye akili yako  kwa mda mrefu, ujue kitu hicho itafika muda utaona matokeo yake yakitokea kwa nje.
Hakuna namna ambavyo unaweza ukaficha, wewe ni matokeo ya vile unavyoviweka ndani yako na sio matokeo ya kitu kingine.

Ubora wa maisha yetu unategemea sana ni kwa namna gani, ambavyo tunajilisha mambo ya aina gani kwenye akili zetu.
Mawazo yanayofanya maisha yetu yabadilike iwe yawe mazuri au mabaya si mawazo mageni sana kwetu, ni mawazo yaleyale ambayo tunakuwa nayo kwa muda mrefu.
Inapotokea ukawa na mawazo ya aina fulani na kwa muda mrefu kwenye akili yako na yakijirudia tena na tena, mwisho wa siku hutokea kwa uhalisia.
Haupo muujiza katika hili hata kidogo, maisha yako yapo hivyo hapo kutokana na mawazo ambayo unayo wewe na umeyashikiria pengine kwa muda mrefu sana.
Kwa hiyo mpaka hapo unaona ni kwa jinsi gani ambavyo unatakiwa kuwa na mawazo tulivu, mawazo ambayo yatakusaidia na si kuweza kukubomoa.
Haijalishi kiwango cha elimu ulichonacho, pesa ulizonazo au umri ulionao, lakini unao uwezo wa kufikiria mawazo yako kwa kwa ubora zaidi siku hadi siku.
Jiulize ni kitu gani ambacho unachagua kufikiri kwa kadri siku zinavyozidi kwenda? Je, unachagua kufikiri mawazo ya faida au ya mawazo yale ya kushindwa kwako?
Ruhusu ndani yako uwe na mawazo mazuri ya kukusaidia. Yale mawazo uliyo ndani, yana uwezo wa kutoka nje na kuleta matokeo uyatakayo.
Kitu ambacho unapaswa kuchukua hatua ili uweze kuleta mabadiliko ya maisha yako ni kwa wewe kuanza kuwa na mawazo ya thamani ndani mwako.
Kila siku hakikisha unaingiza mawazo ya thamani na ya kukusaidia kufanikiwa na si mawazo yale mabovu ya kukurudisha nyuma.
Mawazo haya unaweza kuyapata kwa kujisomea vitabu vizuri au hata kwa kujifunza kupitia watu chanya wenye mafanikio makubwa kukuzidi.
Hauwezi kushindwa katika hili, ni swala la kuamua tu wewe mwenyewe. Ikiwa lakini utashindwa kutengeneza thamani ndani mwako, nakuhakikishia utashindwa.
Hakuna bahati mbaya inayotokea au hakuna maisha ambayo unayapata ni ya bahati mbaya, yote yanatokana na wewe mwenyewe.
Kama nilivyosema uchaguzi ni wako, kuendelea kuingiza mawazo mabovu ambayo yatakupoteza au kuwa na mawazo chanya ya kukujenga.
Kumbuka, mawazo yanayoumba maisha yetu, mawazo yanayotengeneza kufanikiwa au kushindwa ni yale mawazo ambayo tunakuwa nayo kwa muda mrefu ndani mwetu.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.