google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 29, 2018

Sahau Kabisa Hali Hii, Ili Utimize Ndoto Zako.

No comments :
Kila mtu anahitaji mafanikio ya aina fulani kwenye maisha yake, ikiwemo hata wewe unahitaji ufikie mafanikio ya aina fulani.
Pamoja na kwamba wengi wetu wana  kiu kubwa ya kuhitaji kufikia mafanikio ya aina fulani, lakini linapokuja swala la kufanya kazi hapo tena kuna shida.
Kuna wakati unapotakiwa kuweka kazi hasa ili uweze kufanikiwa, utajikuta mwili umechoka na hujisikii kufanya kazi kabisa na kuamua pengine  kutulia.
Hali kama hizo zinakuwa zinatokea sana, kwa hiyo utakuta mtu anajivuta sana katika utendaji wake kitu ambacho husababisha uzalishajji wake unakuwa mdogo.

Ili uweze kufanikiwa na kupata matokeo chanya ya kimafanikio ambayo utaridhika nayo, unahitaji kufanya kazi bila kujali hali yoyote inayotokea ndani mwako.
Unapokuwa na hali ya hisia ambayo unaona kabisa kwa jinsi ulivyo huwezi kufanya kazi, basi tambua hali hiyo inaweza ikakuzuia sana kufanikiwa kwako.
Maisha ya mafanikio hayaendeshwi kwa hisia za mwili wako hata siku moja, yanaendeshwa kwa zile hatua ambazo unazichukua kila siku.
Uwe unajisikia au hujisikii kufanya hicho unachokifanya, unatakiwa kukumbuka kwanza, kuchukua hatua hata kama ni kwa kidogo sana.
Watu wengi wanajiangusha kwenye maisha yao kwa sababu  ya kuongozwa na hisia kama hizi ambazo kila wakati zinasema nao kwamba usifanye saa hivi umechoka.
Unatakiwa uwe jasiri ili kuweza kuzishinda hisia zako ambazo zinaweza kukukwamishwa kwa namna yoyote ile na hapo utakuwa mshindi.
Usipofanya hivyo mwili wako utakuendesha sana na mwisho wa siku unajikuta unaanza kudondokea kwenye kundi la watu wavivu.
Kitu ambacho unachotakiwa kufanya kwa sasa, usikubali hata kidogo kuacha kuchukua hatua kwa sababu eti hujisikii kufanya kile unachokifanya.
Wewe unachotakiwa kufanya ni kuchukua hatua, bila kujali unajisikia au hujisikii. Ukishachukua hatua basi, kama ni hamasa itakuja mbele kwa mbele.
Ukumbuke maisha ya mafanikio yanahitaji uvumilivu mwingi na hilo nalo unatakiwa kulivumulia, lakini usipofanya hivyo utashindwa.
Kumbuka, ndoto zako zitatimia tu, kama utachuka hatua na kutokujali hali hii ya hisia ambayo inatokea ndani mwako.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
Pia kama wewe ni mfugaji wa kuku na unahitaji vifaranga bora, waone DM POULTRY FARM PROJECT kwa huduma ya uhakika. Hawa ni wauzaji wa vifaranga wa kuku aina ya KUROILER, SASSO, PURE KIENYEJI na KUCHI. Kwa mahitaji ya vifaranga wasiliana nao kwa 0767 048 035 au 0686 141097 na wote mnakaribishwa.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,








No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.