google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 21, 2018

KIPAJI CHAKO; Wosia Wa Mafanikio Kutoka Kwa Mama.

No comments :
Ilikuwa ni majira ya saa tisa kamili usiku ambapo ndege,wanyama na viumbe vyote vyenye uhai na visivyo vya uhai vilikuwa havipo duniani kwa muda, mida hiyo viumbe vyote vilikuwa vimelala. Usingizi ndio uliokuwa umetawala nyakati hizo.
Ikumbukwe nyakati hizo hali ilikuwa ni shwari sana, yenye kuhamasisha sana kila kiumbe mwenye pumzi kuweza kufanya tafakari ya jinsi gani atapanga siku yake inayofuata, pia kutafakari mchana wake ulikuwaje kwa siku hiyo.
Mida hiyo nilikuwa nimeamka kwa ajili ya kujisomea, hii ilikuwa ni ratiba yangu ya kila siku kuweza kuamka mida hiyo na kuuanza kujisomea masomo mbalimbali kwani ni muda ambao niliuona na tulivu sana kwangu.
Siku hiyo nilikuwa nimepaanga kurudia kujisomea somo la kiswahili kwani siku ile mchana wake, wakati nikiwa shuleni sikumuelewa vizuri mwalimu wangu, hivyo niliona ni vyema kutumia wasaa huo kuweza kujikumbusha.

Wakati naendelea kujimoea nilimsikia baba yangu akikohoa kwa kikohozi ambacho hata mimi binafsi kiukweli kilinistua sana, baba alikohoa kama mara sita mfululizo hivi pasipo kupumzika. Mara baada ya kukohoa vile nilimsikia baba akiita kwa sauti ya chinichini.
“mke wangu amka nakufa mwenzio”  nikamsikia baba akiendelea kuita tena,
,,,,,,, Mama Ester mke wangu, naomba uamke unisadie nakufa mwenzio,,,,,,,,,,,,,
Sauti ile ya baba ilinifanya niache kuendelea kusoma, kwani iligopesha sana na ukizingatia kwa wakati ule nilikuwa bado mdogo hivyo nilikuwa naogopa sana  hadithi mbalimbali zilizokuwa zinahusu kifo.
mmmmmmmh! Nilishusha pumzi ndefu sana huku akili na mawazo yangu, sambamba  na akili yangu iliwaza vingi visivyokuwa na majibu, hivi baba haya maneno ambayo anayesema ana maanisha nini? Niliwaza mwenyewe.
Mawazo na akili yangu viliganda kwa muda mithiri ya barafu ya mlima kilimanjaro, niliwaza pamoja na ugonjwa huu ambao ulikuwa unamsumbua baba hivi akifa atanisomesha nani? Niliwaza pasipo kupata majibu.
Wakati huo hali ya mama ilikiwa si nzuri  pia, kwani naye kwa  kipindi kile wakati baba  anaumwa mama naye alikuwa ni mjamzito.
Niliendelea kutafakakari mambo mbalimbali pasipo kupata majawabu ya kile nilichokuwa nawaza.
Nilifunika daftari ambalo nilikuwa nasoma kisha kutega maskio yangu kusikiliza sauti na kile kilichokuwa kikijiri chumbani kwa baba kwa mama.
Huku baba angu akiendelea kumwita mama yangu pasipo mafanikio yeyote, ghafla baba akamua kumuita mama kwa sauti ya ukali kidogo, “mama Ester ina maana hunisiki? Nakufa mwenzio!
Sauti ile ya ukali ambayo baba alimuita mama, kwa mbali nilisikia mama akiitaka;
Abeee mume wangu.........
“Mama Ester mke wangu kwa kweli mimi hali yangu siku ya leo naona haipo sawa kabisa hivyo sidhani kama nitapona mke wangu ” sauti ile ya baba yenye kila aina zote  upole na ukarimu zilinifanya niamini ya kwamba baba alikuwa amezidiwa sana usiku ule.
Nini kitaendelea, usikose sehemu ya pili ya simulizi hii ya kusimumua ya wosia wa mama sehemu ya pili…..
0757-909942,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.