google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 24, 2018

Hukuna Kinachoshindikana Kwenye Maisha Yako Ukiamua Hivi…

No comments :
Upo uwezekano mkubwa sana kwa kile unachokifanya pengine unakiona kama hakiwezekani na hauna nafasi tena ya kufanikiwa kwa hicho na hata kwa maisha yako kwa ujumla. Hali hiyo inaweza ikawa inakutokea sana na kujiona wewe si kitu.
Lakini kabla hujakata tamaa naomba nikwambie hivi, kwa vyovyote vile iwavyo mtu pekee ambaye ana uwezo wa kubadilisha maisha yako ni wewe mwenyewe. Kukata tamaa hakuwezi kukusaidia kwa namna yoyote ile zaidi ya wewe kuamua kuchukua hatua.
Maisha ya mafanikio ni matokeo ya kuthubutu sana kuchukua hatua hadi kuweza kufanikiwa kwako. Ikiwa lakini utakuwa unachukua hatua za kukata tamaa hutaweza kufika popote zaidi utaweza kukwama.
Ukiweza kuthubu kila siku na kila wakati hakuna maisha ambayo hutaweza kuyapata. Ngazi ya mafanikio fulani utaifikia tu kama wewe ni mchukuaji wa hatua na hakuna kinachoshindikana juu ya hilo hata siku moja.

Tatizo walilonalo watu wengi ni kule kukaa na kufikiri kwamba maisha yao ya leo jinsi yalivyo na ndivyo jinsi yatakavyokuwepo vivyo hivyo hata kwa miaka ijayo. Hicho unachokifikiri sio sahihi na kinakupoteza kabisa.
Leo unaweza ukawa na maisha mabaya sana, lakini kesho ukumbuke hayawezi kuwa hivyo kama unachukua hatua. Kila siku mpya inakuja na fursa zake, kwa nini ugande na fikra potofu kwa kukariri kwamba maisha yako ya leo ni sawa na ya kesho?
Hutakiwi kuwaza hivyo hata siku moja, chukua hatua za kubadilisha maisha yako, hata kama maisha yako unaona hayabadiliki mara moja, lakini elewa kuna wakati itafika maisha yako hayo yatabadilka hata kama yana hali ngumu sana.
Ndio maana nakwambia hakuna kinachoweza kushindikana kwenye maisha yako kama ukiamua kuchukua hatua za kuthubutu. Watu wote wenye mafanikio wanathubutu, kama itatokea huwezi kuthubu ni ngumu sana kuweza kufanikiwa.
Anza leo kufanya jambo ambalo umekuwa ukilitamani sana kulifanya. Huwezi kulifanya lote zima zima anza kulifanya kwa kidogo kidogo hata kwa mithili ya nukta lakini anza. Kwa kuanza kwako unakuwa ndio unathubutu na kubadilisha maisha yako.
Kile utakachokifanya leo hata kama ni kidogo sana lakini ina nafasi kubwa ya kuweza kubadilisha maisha yako na kuwa bora hata kama huoni matokeo ya ghafla yakitokea. Kikubwa thubutu na chukua hatua.
Unapaswa kuelewa kwamba hakuna kitakachoweza kushindikana kwenye maisha yako kama wewe hautaweza kuchukua hatua za kuthubutu na kuhakikisha ndoto zako zinaweza kutimia. KILA KITU KINAWEZEKANA.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,

No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.