google-site-verification: googleabbfd1327a3af7a3.html

Badili maisha yako sasa kwa kuwa na fikra sahihi.

Kujifunza zaidi juu ya maisha na mafanikio, nakualika kwenye kundi la whats app kujifunza kwa kina. Tututumie ujumbe kwa njia ya whats app kwenda 0687449428 kupata utaratibu wa kujiunga.

Jan 28, 2018

Unahitaji Sana Kuwa Na Jambo Hili, Ili Kupiga Hatua Endelevu Za Mafanikio.

No comments :
Kama kuna kitu fulani hukijui, kuwa na shukrani. Unatakiwa kuwa na shukrani kwa sababu, kwa kutokujua huko inakupa wewe sababu ya kujifunza.
Kama mambo yanakuwa magumu kwako sana, kuwa na shukrani pia. Ugumu huo utakusaidia kuwa jasiri na shujaa mkubwa kwenye maisha yako.
Kama umefika wakati umekimbia changamoto zako, kuwa na shukrani tena. Hapo ni wakati wa kutafuta wakati wa kuweza kujiboresha sana ili wakati mwingine usikimbie changamoto kama hizo.

Kama kuna wakati umechoka kwa kushindwa kendelea kwa sababu huoni mafanikio tena, pia kuwa na shukrani kwani huo ni wakati wa kuwa wa tofauti.
Kama kuna wakati umekosea sana si wakati wa kujuta kupitiliza, kuwa na shukrani kwani makosa hayo hutaweza kuyafanya tena.
Kama kuna wakati umekula hasara kwenye biashara yako, kuwa na shukrani. Kupata kwako hasara kutakusaidia sana kuongeza umakini mkubwa.
Ni rahisi sana kushukuru katika mambo mazuri, lakini si rahisi kuweza kushukutru katika yale mambo ambayo tunaona mabaya kwetu hata kama yana mafundisho tusiyoyaona.
Unatakiwa kuzingatia mabadiliko chanya kwenye kila unachokutana nacho, hata kama kitu hicho kinaonekana hakifai, elewa kuna fundisho la kujifunza.
Shukrani zako ni muhimu sana katika kuweza kubadili mtazamo ule wa kushindwa ulionao na kuleta mafanikio kwa yale utarajiayo.
Ni jukumu lako kuweza kujifunza na kukua kutokana na shukrani ulizonazo. Wewe utakuwa ni watofauti sana ikiwa maisha yako yakiwa amejaa shukrani.
Zipo fursa nyingi ambazo utaziona kupitia shukrani na hata ushirika na ikiwezekana misaada ya watu utapata kulingana na shukrani zako.
Waangalie watu ambao wana shukrani kwenye maisha na wale watu ambao hawana, utakuja kuona watu hawa maisha yao ni tofauti kabisa.
Maisha ya watu wenye shukrani utakuja kugundua yamejawa na utele wakati maisha ya watu ambao hayana shukrani yamajawa na utupu.
Kila siku ianzapo, kumbuka kuanza kumshukuru Mungu, shukuru upo kwenye siku ya kipekee ambayo unaenda kufanya mabadiliko makubwa.
Hiyo haitoshi shukuru pia juu ya kila unachokipata hata kama ni kidogo. Usipokuwa na shukrani hata hicho kidogo unaweza kukikosa.

Msingi wa maisha yako pia unatakiwa kujenga kwenye shukrani hapo pia utakuwa umefanya jambo la maana sana la kuweza kukusaidia.
Fanyia kazi haya na chukua hatua kuhakikisha ndoto zako zinatumia.
Tunakutakia kila la kheri na endelea kutembelea dirayamafanikio.blogspot.com kila siku kujifunza maisha na mafanikio.
Pia rafiki, kama unapenda kujifunza zaidi kuhusu mafanikio, fursa za mafanikio zinapopatikana, ajira pamoja na uwekezaji, karibu kwenye kundi la WHATS APP LA MAFANIKIO, kujiunga tuma neno THE UNIVERSITY OF WINNER’S kwenda 0713 048 035, hapo utapata utaratibu mzima wa kujiunga.
DAIMA TUPO PAMOJA MPAKA MAISHA YAKO YAIMARIKE,
Ni wako rafiki katika mafanikio,
Imani Ngwangwalu,
Mshauri wa mafanikio, mwandishi na mjasiriamali,
Mawasiliano; +255 767 048 035, +255 713 048 035,





No comments :

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.